Monday, 7 November 2016

PICHA: Mwanamke aliyekaa siku nzima kwenye Jeneza ili kupata uzoefu wa kifo.

 

 Imetokea Brazil na Mwanamke mwenyewe anaitwa Vera Lucia da Silva na umri wake ni miaka 44 ambapo aliamua kukaa kwenye jeneza siku nzima ili apate uzoefu wa mazingira ya kifo ili siku akifa asiwe mgeni na Jeneza.

Vera aliamua kukaa kwenye jeneza huku familia yake ikifanya vitu vinayofanywa kwenye msiba ili aone inakuaje ambapo baada ya kutoka humo alisema ilikua siku nzuri zaidi kwenye maisha yake yote.
Sherehe hiyo ya kujifunza maisha ya kwenye Jeneza ambayo ilifanyika Jumatano ya November 2 2016 ni sherehe ambayo ilifanyika kwenye eneo la makaburi.



 Ndugu zake walipingana sana na wazo lake lakini baadae waliamua kukubaliana naye na kuvaa nguo nyeusi wakati walipomtembelea na kufanya kama wanatoa heshima za mwisho




  

Mmiliku wa eneo la kuzikia liitwalo Eternal Garden Funeral home, Paulo Araujo, aliamua kumpa Jeneza Vera bila gharama zozote, kama mgeni maalumu.
Wakati akiwa ndani ya Jeneza mwanamke huyo alikua akifumbua macho na kufumba kama vile mtu aliyekufa na kufufuka.





 Mwanamke huyo amesema alikuwa na ndoto ya kulala kwenye Jeneza tangu miaka 14 iliyopita na hakuwa akifikiri ingekuja kutokea akaitimiza, kwasasa amefurahi kutimiza alichokitaka kabla hajafa.

alicho zungumzia Diana kabla hajashinda taji la kua miss tz





Miss tanzania ilivyokua jijini mwanza



                   

Friday, 4 November 2016

Ochu wetu

Azam FC yapata pigo kwa kumpoteza kiongozi wao

 

November 7 2016 taifa la Tanzania limepata pigo kwa kupokea taarifa za kifo cha mbunge wa zamani wa Urambo na Spika wa bunge wa zamani mzee Samuel Sitta, baada ya taarifa hizo  kuenea zimeripotiwa taarifa nyingine za klabu ya Azam FC kumpoteza aliyekuwa mwenyekiti wao Said Mohamed.
Mzee Said Mohamed amefariki November 7 2016 akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Agakhan Dar es Salaam, mzee Said alikuwa na mchango mkubwa katika soka sio  tu ndani ya klabu yake ya Azam FC.
Kama utakuwa unakumbuka vizuri mzee Said Mohamed alikuwa meneja mkuu wa makampuni ya SSB, mwenyekiti wa Azam FC, makamo mwenyekiti wa bodi ya Ligi na mjumbe wa kamati ya utendaji ya shirikisho la soka Tanzania TFF.






 
 Mwenyekiti wa Azam FC na meneja mkuu wa makampuni ya SSB Said Mohamed amefariki dunia leo akiwa katika hospitali ya Agakhan Dar es Salaam

Wednesday, 2 November 2016

Yanga wakubali kipigo cha pili msimu huu dhidi ya Mbeya City By Rama Mwelondo TZA on November 2, 2016 Share Tweet Share Share comments Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania bara, leo November 2 2016 walishuka katika uwanja wa Sokoine Mbeya kucheza dhidi ya wenyeji wao Mbeya City katika mchezo wao wa 13 wa Ligi Kuu Tanzania bara msimu wa 2016/2017. Yanga wakiwa ugenini huku wakiwa na kumbukumbu ya kipigo chao cha kwanza kutoka Stand United cha goli 1-0 September 25 2016, leo November 2 2016 wamekubali kipigo cha pili kutoka kwa Mbeya City wakiwa katika dimba la Sokoine Mbeya. img-20161102-wa0049 Mbeya City wamefanikiwa kuifunga Yanga goli 2-1, magoli ambayo yalifungwa na Mwasapili dakika ya 6 na Kenny dakika 36 goli ambalo lilichukua muda kidogo refa kufanya maamuzi kutokana na wachezaji wa Yanga kuligomea, Donald Ngoma ndio alifunga goli la kufutia machozi la Yanga dakika 4 za nyongeza kabla ya kwenda mapumziko.